Ebenezer Television ni kituo kipya cha habari ambacho kinatarajia kuanza kurusha matangazo yake kutokea Mikocheni Dar es Salaam. Kituo kinahitaji wafanyakazi katika Nyanja zifauatazo;

A.    NAFASI ZA AJIRA

1.     Mhariri Mkuu – Nafasi moja (1)
-        Awe na Shahada ya Uandishi wa Habari au Mawasiliano ya umma
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka mitatu katika nafasi hiyo
-        Awe amelelewa katika maadili ya kikristo.
-        Awe na uwezo wa kusimamia uzalishaji wa vipindi
-        Awe amehitimu katika vyuo vikuu vinavyotambulika na serikali.

2.     Wazalishaji vipindi – Nafasi tatu (3)
-        Awe ana kiwango cha chini cha Stashahada kutoka Chuo kinachotambulika.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika nafasi hiyo

3.     Waandishi wa Habari – Nafasi tatu (3)
-        Awe ana kiwango cha chini cha Stashahada kutoka Chuo kinachotambulika.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika nafasi hiyo

4.     Wahariri wa picha nyongefu na wasanifu – Nafasi mbili (2)
-        Awe na Stashahada kwenye uandishi wa habari, uhariri picha au ubunifu wa matangazo.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

5.     Wapiga picha nyongefu – Nafasi nne (3)
-        Wawe na elimu kuanzia Astashahada katika upigaji picha nyongefu
-        Awe na ujuzi wa sauti za picha nyongefu
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

6.     Warusha Matangazo – Nafasi tatu (3)
-        Awe na Stashahada katika teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT)
-        Au Stashahada katika teknolojia ya mawasilianao na elektroniki
-        Awe na uwezo wa kutatua matatizo ya kiufundi
-        Awe na uwezo wa kushauri vifaa bora kutokana na teknolojia

7.     Wasoma Habari – Nafasi tatu (3)
-        Awe na elimu isiyo chini ya Astashahada ya Uandishi wa Habari au sifa inayofanana na hiyo.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika fani husika

8.     Mkutubi – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyo chini ya Astashahada ya utunzaji kumbu kumbu
-        Awe ana ujuzi wa kutunza vielelezo vya sauti na picha nyongefu
-        Uzoefu wa zaidi ya mwaka mmoja.

9.     Msimamizi wa vipindi – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyopungua astashahada ya uandaaji na usimamizi wa vipindi
-        Awe anajua kupanga ratiba za vipindi katika kituo cha runinga.
-        Awe anajua kupanga utaratibu wa matukio ya kitaifa au kikanisa yatakayotokea.
-        Awe anajua kupanga na kuratibu matangazo ya biashara katikati ya vipindi pale endapo tangazo litakuja.

10. Mratibu wa maudhui mtandaoni – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyopungua Astashahada
-        Awe na uzoefu wa mitandao ya kijamii
-        Mwenye ujuzi wa mifumo ya kielectronika na komputa

11. Msimamizi wa Utawala – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu ya shahada ya awali katika Uongozi yaani (Public Administration, Leadership and Governance.
-        Mwenye ujuzi wa habari na Mawasiliano atapewa kipaumbele
-        Awe amelelewa katika maadili ya dini ya KIKRISTO
-        Awe tayari kufanya kazi nyingine zinazoendana na nafasi hyo
-        Awe na uwezo wa kufanya tathmini ya wafanyakazi waliopo na kushauri Uongozi njia bora ya kuboresha.
-        Uzoefu wa miaka miwili katika nafasi kama hyo

12. Mhasibu – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu ya shahada ya awali katika masuala ya fedha
-        Awe amelelewa katika maadili ya kikristo
-        Awe na uelewa katika masoko na biashara
-        Awe na uzoefu wa miaka miwili
-        Awe amelelewa katika maadili ya KIKRISTO

13. Fundi sanifu wa umeme – Nafasi moja (1)
-        Awe na stashahada ya umeme katika chuo kinachotambulika
-        Awe na uzoefu wa vifaa vya electronics na sauti
-        Awe anaufahamu umeme wa phase moja na phase tatu
-        Awe na uwezo wa kufuatilia tatizo la umeme na kulitatua
-        Awe na ujuzi wa kuunganisha na kuwasha generator.



B.    NAFASI  ZA WAKURUFUNZI (INTERNS)
1.     Waandishi wa Habari – Nafasi tatu (3)
2.     Mhariri wa picha – Nafasi mbili (2)
3.     Msaidizi wa msimamizi wa vipindi – Nafasi mbili (1)
4.     Mrusha Matangazo – Nafasi mbili (2)
5.     Wapiga picha – Nafasi mbili (2)
6.     Wakutubi – Nafasi mbili (1)
7.     Waandaaji vipindi – Nafasi mbili (2)

-        Wawe na ujuzi katika fani husika uzoefu si lazima AU awe mwanafunzi anayetarajia kumaliza masomo katika fani husika

C.    Watendaji wa kujitolea (Volunteers)
1.     Wapiga picha – Nafasi 1
2.     Wahariri picha – Nafasi 3
3.     Waandaaji vipindi – Nafasi 4
4.     Afisa Masoko – Nafasi 3


Maombi yote yaliyo ambatanishwa na nakala za vyeti na CV yatumwe kwa;
Mratibu wa Mradi - Ebenezer Television
S.L.P 4067
Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Dar es Salaam.

AU

Kwa barua pepe ebztvtz@gmail.com katika mfumo wa PDF na viambatanisho vyote viwe katika nakala moja. Mwisho wa kutuma maombi ni February 12, 2020.