Ad Code

Responsive Advertisement

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 18.12.2019: Pogba, Haaland, Ancelotti, Ronaldo, Kante


Paul Pogba
Manchester United hawatamruhusu kiungo wao Mfaransa Paul Pogba, 26, kuihama klabu hiyo katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari. (Mail)
United inaamini kuwa itamsajili mshambuliaji nyota wa Red Bull Salzburg na timu ya taifa ya Norway Erling Braut Haaland kwa kitita cha pauni milioni 76 mwezi Januari - na endapo wataruhusu mchezaji huyo asalie kwa mkopo Salzburg mpaka mwisho wa msimu. (Sun)
Hata hivyo klabu ya Red Bull Leipzig pia wamempatia ofa mpya kwa minajili ya kumshawishi mshambuliaji huyo mwenye 19 kusalia klabuni hapo. (Kicker, via Mail)
Haaland
Carlo Ancelotti atambakiza kocha wa muda wa Everton Duncan Ferguson kama sehemu ya benchi la ufundi kama atateuliwa kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo. (Telegraph)
Ajenti wa Cristiano Ronaldo, bwana Jorge Mendes amedokeza kuwa nyota huyo mwenye miaka 34 huenda akamaliza maisha yake ya kandanda katika klabu ya Juventus. (Sky Sports, via Goal)

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DEC 18 2019
Manchester City wamewapiku Manchester United katika mbio za kutaka kumsajili beki kinda wa Barcelona Juan Larios, 16, mwezi Januari. (Record)
Kante
Barcelona hawana mipango ya kumsajili kiungo mkabaji wa klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya Ufaransa N'Golo Kante, 28. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Klabu za Ligi ya Primia Liverpool, Manchester United na Chelsea wamepatwa na pigo baada ya winga raia wa Ujerumani Kai Havertz, 20, kubainisha kuwa anataka kubaki katika klabu yake ya Bayer Leverkusen inayoshiriki ligi ya Bundesliga. (Sky Sports)
Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 17.12.2019: Arteta, Ancelotti, Young, Dembele, Ibrahimovic 
Crystal Palace wataendelea kumthaminisha mshambuliaji wao raia wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 27, katika dirisha dogo la usajili la mwezi Januari. (Mail)
Kocha wa zamani wa Newcastle na Liverpool Rafa Benitez, ambaye kwa sasa anaifundisha klabu ya Uchina ya Dalian Yifang, amesema ipo siku atarejea Ligi ya Primia. (The Athletic)
SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DEC 18 2019
Reactions