Ad Code

Responsive Advertisement

Uganda kuwatoza ada wanaotaka kufanyiwa vipimo vya corona

IBM's response to the COVID-19 coronavirus - Denmark | IBM

Uamuzi wa serikali ya Uganda kuza watu ada ya kufanyiwa kwa hiari vipimo vya Covid-19 huenda vikaathiri usafiri kurejelewa kwa shughuli za utalii na biashar kwaHatua hiyo pia huenda ikawaathiri raia wa Uganda wanaorejea nyumbani kutoka ughaibuni.

Jumapili iliyopita ,serikali ilitoa muongozo unaozitaka mashirika kutoza watu dola 65kufanyiwa vipimo vya corona.

Mashirika yanayopanga kuwafanyia vipimo wafanyakazi wao ama watu binafsiambao wanataka kubaini ikiwa wameambukizwa virusi vya corona pia watalazimika kulipa.
Mamlaka mjini Kampala inasema ada hiyo itachangia kugharamia mpango wa kukabiliana na janga la corona.

Kufikia sasa watu 350,000 wamefanyiwa uchunguzi, na 2,900 kati yao wamethibitishwa kupata maambukizi huku vifo vya watu 30 vikirekodiwa.
Watu walioonesha dalili ya maambukizi ama wale waliotangamana na wagonjwa wa corona, hawatatozwa ada yoyote.

Kuna hofu ada hiyo huenda ikahujumu juhudi zilizopigwa katika mapambano dhidi ya maambukizi ya corona.

Pia huenda ikaongeza gharama ya uagizaji bidhaa kutoka nje ya nchi kwasababu madereva wa malori watalazimika kulipia vipimo.

BBC
Reactions

Post a Comment

0 Comments